Social Icons

Ijumaa, 23 Mei 2014

FAHAMU MATUMIZI YA ASALI KWA UPONYAJI WA MISHONO YA OPERATION.

 

ASALI ni dawa nzuri sana katika kutibu mishono ya operation mbali mbali. Wataalamu wanazidi kuhamasisha matumizi ya asali kwenye mishono kila siku.
Asali Imekua inatumika kwa miaka mingi kwasababu zifuatazo:-

1. Ina kiwango kikubwa cha sukari ( High Sugar content) inayofanya bakteria washindwe kuzaliana au kuishi.

2. Ina kiwango kidogo cha unyevu ( Low Moisture content) - hii inafanya kidonda kiwe kikavu

3. Ina HYDROGEN PEROXIDE ambayo inazuia bakteria

4. Gluconic acid ambayo inatengeneza mazingira ya Acid kwenye kidonda na hivyo kuzuia ukuaji wa bakteria.

Faida ya kutumia ASALI kwenye mishono ya operation ni pamoja na:-

1. Inapunguza kuvimba kwa kidonda na pia uvimbe wa kidonda

2. Inaongeza spidi ya uponaji wa kidonda.

3. Inasafisha kidonda

MATUMIZI YAKE
Unaweza paka hadi mara mbili kwa siku kuharakisha uponaji, lakini hakikisha asali hiyo ni safi.

ANGALIZO
Unashauriwa upate ushauri wa kitaalamu kwanza wa daktari wako kabla ya kujiamulia kupaka mwenyewe nyumbani ili kufanya kitu sahihi.

Tafadhali naomba TUSHARE kwa wingi sana ili watu wengi waipate elimu hii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni