Social Icons

Ijumaa, 14 Februari 2014

JE UNAJUA KWA NINI TUNAFUGA NYUKI, SOMA HAPA KUPATA UFAHAMU

KWANINI TUNAFUGA NYUKI

Fuatilia muendelezo wa maelezo toka FANO 2010 Products kujua mhuhimu wa kufuga nyuki.

Tokea zama za kale binadamu wamekuwa wakitafuta asali inayozalishwa na nyuki. Kwa azma hiyo shughuli yoyote ya ufugaji nyuki ni kuendeleza zaidi ufanisi wa haya.

 Binadamu na nyuki hutegemeana. Kwani kwa upande wa nyuki badala ya kuwindwa na kuuawa kwa ajili ya asali yao hutunzwa na kulindwa. Matokeo ya haya siyo tu kupatikana kwa asali na nta bali pia kutambuliwa kwa nyuki kama rasilimali muhimu ya kuhifadhiwa kulindwa na kustawishwa.

Ukusanyaji wa asali na nta ni shughuli ya kijadi katika karibu bara lote la Afrika. Wafugaji nyuki wa jadi hutumia mizinga rahisi ambayo njia ya uvunaji asali huluta maangamizo ya makundi ya nyuki.

Kwa hiyo iko haja ya kubadilisha njia hii kali ya ufugaji nyuki na kuanzisha ufugaji nyuki mzuri wenye ufanisi zaidi. Huu ni ufugaji wa kutumia mizinga ya masanduku yenye viunzi vya juu au masanduku yenye fremu.
Shughuli yenyewe inaweza ikawa ni mradi wa kiwango kidogo ambao unaweza kuendeshwa kirahisi. Nyuki wanasaidia kuchavusha mimea ya asili na ile ya kilimo na biashara. Mizinga haichukui eneo lolote la ardhi na haitegemei pembejeo kutoka nchi za nje. Yeyote anaweza akaanza ufugaji nyuki na familia nzima ikaweza kushirikishwa. Njia nzuri ya kujifunza juu ya ufugaji nyuki ni kufanya kwa vitendo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni